#Kitabukipya: Faragha ya Kiroho sasa kipo sokoni.
Mwandishi wa vitabu na mwangalizi wa Bread of Life Teaching Ministry, Meinrald A. Mtitu ametoa kitabu kingine - Faragha ya Kiroho. Ametuandikia kipande kidogo kuhusu kitabu chake, anasema kwamba;
Mazoezi ya kiroho yanaelezeka kama tabia na mazoea yanayowezesha kukua kiroho. Ukitaka kukua kiroho kwa haraka fanya mazoezi ya kiroho mara kwa mara. Mazoezi ya kiroho unayo yafanya kwenye faragha yako ya kiroho yana kuleta karibu na Mungu na kukufanya kuwa mtauwa zaidi katika tabia na mwenendo wako, yanabadilisha maisha yako siku kwa siku. Katika 1 Timotheo 4:7 , tunaona Paulo anamwambia Timotheo “ajizoeze kuwa mtauwa”. Tafsiri ya ya Biblia ya NIV, na ya NKJV inasema “fanya mazoezi ya kuwa mtauwa”. Timotheo anaambiwa hivi, kama vile mwanariadha anavyoufunza na kuuzoeza mwili wake, hivyo ndivyo na yeye anavyolazimika kuifunza nafsi yake kwaajili ya utauwa. Paulo anaeleza juu ya uthamani na faida za mazoezi haya kiroho, kwa maneno haya, “ mazoezi ya kimwili yanafaa kidogo lakini mazoezi ya kiroho yanafaa zaidi. (1 Timotheo 4:8).
Mazoezi ya kiroho yanaturuhusu sisi kujiweka mbele za Mungu ili kwamba aweze kutugeuza. Jukumu letu ni kutengeneza maisha yetu ya kila siku katika udongo wenye rutuba ambao Mungu ataleta kukua na mabadiliko, hiki ndicho mazoezi ya kiroho yanamaanisha”. Yafuatayo ni baadhi ya mazoezi ya kiroho unayoweza kuyafanya katika faragha yako ya kiroho; Zoezi la kiroho la ukimya, zoezi la kiroho la maombi, zoezi la kiroho la kutafakari,zoezi la kiroho la kujifunza neno, zoezola kiroho la kuabudu na zoezi la kiroho la kufunga na mengineyo.
Kitabu hiki kinakupa mafundisho mazuri yenye kukuongoza vile unaweza kuanza kuwa na nidhamu ya kwenda mahali pako pa siri kwaajili ya kufanya mazoezi ya kiroho ambayo yatakusogeza karibu na Mungu zaidi na kukubadilisha zaidi. Kisome kitabu hiki tena na tena, kisha anza kuyatendea kazi mazoezi ya kiroho katika vipindi vyako vya faragha ya kiroho. Ni hakika baada ya kusoma kitabu hiki hautabakia vile ulivyokuwa kabla, kuna hatua mpya na viwango vipya utavyopiga. Mungu akubariki sana kwa kusoma kitabu hiki.
Unaweza kuweka oda hapa chini.