Mahusiano na wakati
Katika kitabu hiki nimejaribu kuelezea mambo nyeti yanayokumba vijana hasa mahusiano ya kimapenzi, Biblia inatoa mwongozo wa maisha ya kila rika, mahusiano ya kijamii katika rika mbali mbali, alafu inatoa mwelekea wa kuiingia mbingu. Biblia inaonyesha tamaduni, mila na desturi za kiMungu katika tamaduni, mila na desturi za wanadamu.
Ikumbukwe kabla ya Biblia kudhihirishwa katika maandiko wanadamu waliishi katika mila na tamaduni zao. Lakini cha ajabu sana Mungu alishaweka mwongozo wa maadili ya kila binadamu katika dhamiri yake warumi ……….(dhamiri ni sauti ya binadamu ya ndani, ni msukumo wa ndani wenye kushtaki mtu anapofanya kisichosawa katika jamii iliyokubaliana juu ya utaratibu flani au mbele za Mungu hata kama mtu huyo hamjui Mungu.
Sasa kuna ulimwengu wa aina mbili, ule unaoenenda kama unavyotaka kwa kuzifuata tama za anguko na ule unaofuata maadili ya Mungu. Sasa kwa Yule anayetaka kutembea katika maadili ya Mungu lazima afuate kile Mungu anasema.
Katika kamusi ya Mungu hakuna kitu hiki kinachoitwa “kuwa na mpenzi wako wakati huo mnasubiri umri ukifika muoane au msioane vyovyote (courtiship). Japo ulimwengu wa wasiofuata maadili ya biblia (yaani mwongozo wa Mungu wanaishi kwa maisha na mwongozo wa aina hiyo.
Others Also Bought