Nguvu ya Urafiki
Kitabu hiki cha “Nguvu ya Urafiki” kinaelezea zaidi kuhusu urafiki na matokeo yake katika maisha yetu. Kila mtu ana rafiki au amewahi kuwa na rafiki, hivyo basi, hiki ni kitabu kinachohitajika na watu wa kila rika. Urafiki ni jambo la hiari na siyo la kulazimisha (Friendship is an optional matter and not by force), kila mtu huwa anachagua ni aina gani ya rafiki anataka kuwa naye katika maisha.
Watu wengi wamepoteza dira ya maisha yao kutokana na marafiki. Pia, kuna wengi wamefanikiwa sana katika maisha yao kutokana na marafiki. Hivyo basi, kitabu hiki kitakusaidia sana kujua nani ni rafiki wa kweli, namna ya kuchagua rafiki wa kweli, kujua kile kitu ambacho rafiki anaweza kufanya katika maisha yako, urafiki kati ya mume na mke, mzazi au mlezi na mtoto na Faida za urafiki na Mungu.
Pia, maudhui ya kitabu hiki yataenda sawia na shuhuda mbalimbali za watu waliopata matokeo chanya au hasi kutokana na marafiki. Ni matumaini yangu kwamba ndugu msomaji hutajuta kupata nafasi ya kusoma kitabu hiki, na Mungu akusaidie uweze kukisoma mpaka mwisho na kumshikirisha mwingine baraka na maarifa haya. Mungu akubariki sana
Recommended for you

-23f6fae7.jpg?7122581)

