Skip to main content
DL Bookstore
  • Home
  • Get books
  • Author services
  • Courses
  • Blog
  • Support
  • All books
  • Discounts
  • Swahili books
    • Dini
    • Fasihi
    • Maendeleo binafsi
    • Malezi
    • Ndoa na mahusiano
    • Uchumi na biashara
    • Uongozi na usimamizi
    • Vitabu vya kiada
  • English books
    • Business and finance
    • Literature
    • Parenting and relationships
    • Personal development
    • Religion and spirituality
    • Textbooks
  • Children's books
  • Online courses
  • Free books
  • Get books
  • Swahili books
  • Ndoa na mahusiano
  • Una Wito wa Ndoa Kabla ya Ndoa?

Una Wito wa Ndoa Kabla ya Ndoa?

TZS 10,000
Add to cart  

NDOA ndio taasisi kongwe zaidi kuliko hata DINI iliyokusudiwa na Mungu idumu milele. Ni agano linalomuunganisha mtu MUME na mtu MKE kiroho na kimwili katika KUTIMIZA KUSUDI LA MUNGU ndani yao. 

Najua umeshawahi kujiuliza kwa nini leo hii tunashuhudia MIGOGORO mingi katika taasisi hii takatifu ya ndoa? Kuna sababu nyingi sana zinazoweza kupelekea wanandoa kuachana (TALAKA) ama kuuana, lakini sababu mojawapo kubwa ni ukosefu wa UFAHAMU na MAARIFA kuhusu MAHUSIANO na NDOA kwa ujumla wake.

Ukweli ni kuwa wengi wetu tumejengewa mawazo kuwa maisha ya ndoa ni ya matatizo tu, naamini hata leo hii bado wengi wanafikiri hivyo, wamepokea hivyo, ndio maana kila anayeoa au kuolewa lazima aambiwe kuwa nenda kavumilie. Sijui wewe rafiki yangu uliambiwaje? Sikiliza, si mpango wa Mungu ndoa iwe sehemu ya mateso au iwe ni sehemu ya matatizo yanayopelekea watu kukosa amani na hata kupata magonjwa na kufa; au kushindwa kumtumikia Mungu wao.

Niliamua kuandika kitabu hiki kwa ajili ya wale wote wanaojitayarisha kufunga ndoa, wale walio kwenye ndoa tayari, na kwa yeyote anayetamani kupata ufahamu zaidi kuhusu maisha ya ndoa. Kwa sababu tunaishi katika siku ambazo talaka zimekuwa nyingi na utata mwingi kuhusu suala hili.

Ni tumaini langu kupitia kitabu hiki nitaweza kukusaidia kuchochea imani yako na uhakika wa maisha mazuri yenye upendo kwa wale ambao bado hawajaanza safari ya ndoa na wale walio tayari katika ndoa. Nakutia moyo tena kuwa inawezekana tena kutengeneza upya hadithi yako nzuri katika maisha ya ndoa kwani NDOA NI MPANGO ASILI WA MUNGU!

NAMALIZIA kwa kukumbusha kuwa pamoja na yote ambayo umekuwa unayasikia na kuyafahamu kuhusu ndoa, lakini niamini NAPOKWAMBIA kuwa ndoa ni nzuri hasa kama MWANAUME (mtu mume) na MWANAMKE (mtu mke) watajifunza na kuzifuata KANUNI ZA ASILI (Laws of nature) kabisa zilizowekwa na Mungu mwenyewe kuhusu taasisi hii kongwe kuliko zote DUNIANI.


Others Also Bought

Ndoa si Ndoano
Ndoa si Ndoano
TZS 10,000
Add to cart
Fahamu Misingi na Kanuni za Ndoa
Fahamu Misingi na Kanuni za Ndoa
TZS 15,000 TZS 10,000
Add to cart
Mahusiano bora kabla na ndani ya ndoa
Mahusiano bora kabla na ndani ya ndoa
TZS 7,500 TZS 4,000
Add to cart
Ushauri wa Ndoa katika Mtazamo wa Kibiblia
Ushauri wa Ndoa katika Mtazamo wa Kibiblia
TZS 10,000
Add to cart

Cart

Cart is empty.

Log in

Incorrect password.




Forgot password?
Create an account
Login to existing account
My orders
My reviews
My details
Log out
  • Home
  • Get books
  • About us
  • Author services
  • Blog
  • Support
  • Client portal
DL Bookstore © 2025. All rights reserved.