Akili Iliyoponywa Kuhusu Fedha
Hata serikali ya Muungano wa Tanzania ikiamua kuchukua mali zote za matajiri na kuamua kuwagawia watu wote na maskini kwa usawa kitakachotokea baada ya mwaka mmoja ni tajiri kubaki tajiri tena na masikini atabaki kuwa masikini tena.
Watu wengi wakipata pesa hukimbilia kununua gari wakidhani tabia ya mtu kuonekana ana pesa ni kuwa na gari, hapana, si kweli, usinunue gari ikiwa bado hujawekeza baadhi ya mali. Wekeza mali nyingi sana kwa sababu zitakupa pesa nyingi ambazo zitakurahisishia kununua gari bila kupata maumivu. Gari itakusaidia kwenye usimamizi wa mali ulizowekeza.
Nakushauri uwe na busara unapopata pesa. Ikiwa mshahara wako ndio chanzo pekee cha mapato yako, hiyo ni hatua ya kuelekea umaskini. Weka akiba katika kila mapato na utumie akiba hiyo kuwekeza. Soma kitabu hiki ukurasa hadi ukurasa usiruke, baada ya kukamilika kwa kitabu hicho utapata uzoefu wa kiwango kingine cha maisha yako
Recommended for you




