Skip to main content
DL Bookstore
  • Home
  • Get books
  • Author services
  • Courses
  • Blog
  • Support

Jarida la bure | Maisha Jinsi Tuyajuavyo

May 23, 2020 at 9:33 am,


Mshairi wa uingereza W.H .Auden anasema "tumewekwa duniani kusaidia wengine lakini kile wengine wamewekwa kukifanya siwezi kusema". Watu wengi hufikia hatua ya kukata tamaa na kushindwa kabisa kustahimili  nilimsikia mtu mmoja akisema "Nimedhoofika sana,nimeumwa sana maisha yangu yamekuwa ya mateso mno hapa duniani ,nikapumzike tu. Huzuni na dhiki haitakuwepo tena,sitaomba omba mahitaji"


Watu wengi hufikia hatua ya kukata tamaa na kushindwa kabisa kustahimili  nilimsikia mtu mmoja akisema "Nimedhoofika sana,nimeumwa sana maisha yangu yamekuwa ya mateso mno hapa duniani ,nikapumzike tu. Huzuni na dhiki haitakuwepo tena,sitaomba omba mahitaji"

Kamwe tusimpite mtu anayeteseka bila kujitahidi kumpa faraja,kama sisi tulivyopewa tulipokuwa katika hali hiyo. Kuna mengi yakutunyong'onyeza, na kutufanya tuhisi upweke mkubwa mno. Magonjwa yanatufanya kuwa dhaifu sana, unaweza kuwa mzima leo, kesho ukawa kitandani hoi ,unapigania maisha.


Kuna wakati tunapitia magumu mengi  ya kutisha kiasi cha kushindwa kujua tufanyaje zaidi ya kuwa na hofu .Hatujui kesho yetu imebeba nini ? tutakuwa wapi ? tutakuwa na hali gani?  nani atakushika mkono na kurejesha lile tumaini angavu? . Mwinjilisti Pascal Cassian anasema " Hakuna mtu anayejua kesho yake,hata mimi sikujua kama ningekuwa hivi ,kama ningelijua nitakuwa hivi ningejiandaa,ningeweka akiba nisije ombaomba"

Mwandishi Joyce Mayer anasema "Hebu fikiria jinsi ambavyo ulimwengu, ungelikuwa na tofauti iwapo kila mmoja wetu angefanya jambo la ukarimu kwa mtu fulani kila siku . Matokeo yake yangekuwa ya kushangaza.Ulimwengu ungebadilika haraka..Fanya sehemu yako watu wengine watafanya sehemu yao.Usikubali ushindwe kupitia kufikiri kabla hujaanza."

Ukiwa kweli unataka kitu fulani chenye manufaa kwa watu wengine ,utatafuta njia ya kufanya.Hakuna zawadi ya kutofanya lolote ,fanya kitu.Huwezi kuwa masikini kwa sababu tu ya kuwasaidia wengine.Usiseme huna uwezo wa kuwa shughulikia watu wengine sababu labda kipato chako ni kidogo . Mama Teresa anasema"hakuna mtu ambaye ni masikini mpaka hana kitu cha kutoa...". Kama uwezi kufanya mambo makubwa wewe mwenyewe ,kumbuka unaweza kufanya mambo madogo kwa maana kubwa.Kuna mambo mengine mengi ,muhimu na ya thamani unayoweza kufanya yenye mguso mkumbwa kwenye maisha na kuleta tofauti ifaayo ulimwenguni kupitia mambo madogo madogo ."Tumia resilimali zako ,zaidi ya pesa .Resilimali zetu ni pamoja na nguvu , wakati ,vipawa,na mali tulizonazo"anasema Mwandishi wa mageuzi ya upendo Joyce Mayer........

BURE BURE BURE BURE…JIPATIE JARIDA LETU LA MAISHA JINSI TUYAJUAVYO TOLEO LA PILI JIHUSISHE FANYIKA BARAKA. BURE ILIKULIPATA

WASILIANA NASI 0624006306 au email maishajinsituyajuavyo@gmail.

Ubunifu wa jalada na mpangilio wa ndani wa jarida hili umefanywa nasi DL Bookstore. Angalia huduma zetu HAPA

Kununua vitabu vya kusoma tembelea HAPA




Recent Posts

  • Download Vitabu 7 vya Fedha (PDF)
    19 Jun, 2025
  • Kutoka Daftari Hadi Kitabu Halisi: Jinsi ya Kugeuza Maandishi Yako Kuwa Kitabu
    16 May, 2025
  • Umechoka na Minyama Uzembe? Suluhisho la Kupungua Uzito Limepatikana!
    17 Apr, 2025
  • Vitabu Bora vya Pasaka vya Kukuimarisha Kiroho – Vinapatikana Sasa DL Bookstore
    11 Apr, 2025
  • 4 Benefits of Selling Your Book Through DL Bookstore
    20 Mar, 2025
  • Download Entrepreneurship Books (PDF) in Swahili
    10 Feb, 2025
  • Download Nine (9) Must-Read Books for Girls and Women 📚✨
    4 Feb, 2025

selling_book-1.png

Enroll in 100% free courses

100% free courses on writing, publishing, and marketing of books. Time to dive in!

Start learning →

Cart

Cart is empty.

  • Home
  • Get books
  • About us
  • Author services
  • Blog
  • Support
  • Client portal
DL Bookstore © 2025. All rights reserved.