Huduma ya Ushauri Katika Mtazamo wa Kikristo
Kitabu hiki kimeaandika ilikukabiliana na uhitaji mkubwa wa mafunzo ya ushauri. Kumekuwa na wimbi kubwa la uendeshaji wa huduma za ushauri , na washauri wengi hawajapata nafasi ya kupata mafunzo rasimi ya ushauri. Lakini wamekuwa wanafanya kazi kubwa sana ya kusaidia maisha ya watu wengi wanaopitia matatizo mbalimbali ya kiroho, kihisia, kiakili na kimwili.
Msukumo, mzigo na wito na karama ya kuwasaidia wengine katika kutoka kwenye matatizo yao ni msingi katika huduma ya ushauri, lakini hata hivyo hatuwezi kupuuzia umuhimu wa kufanya ushauri kama taalamu rasmi. Hivyo basi ni muhimu huduma ya ushauri ifanywe kwa kuzingatia vigezo vyote muhimu vya kitaaluma.
Katika kitabu hiki kuna maarifa mengi muhimu ya kuwasaidia watumishi wanaofanya huduma ya ushauri ili waweze kuifanya kwa ufanisi na umahiri. Maeneo muhimu yaliyogusiwa ni kama vile Misingi ya huduma ya ushauri, Aina mbalimbali za ushauri, Njia mbalimbali za kufanya ushauri, Ushauri na Theolojia, Ushauri na Saikolojia, Sifa za mashauri, Maadili ya kufanya huduma ya ushauri, Kanuni na Ujuzi wa ushauri, Hatua za kufanya ushauri na mengine mengi.