IMANI ILIYO HAI KATIKA ULIMWENGU WENYE KELELE
Katika ulimwengu wa sasa uliojaa kelele – kelele za mitandao ya kijamii, mafundisho ya uongo, hofu za kiuchumi, vita vya kiroho, na mivurugiko ya kimaadili – waumini wengi wanapitia kipindi kigumu cha kudumisha imani iliyo hai. Kitabu hiki ni mwongozo wa kiroho unaoelekeza namna ya kuitunza na kuikuza imani ya kweli ya Kikristo katikati ya machafuko ya dunia ya sasa.
IMANI ILIYO HAI KATIKA ULIMWENGU WENYE KELELE ni kitabu kinachoeleza:
- Tofauti kati ya imani ya kweli na imani ya mazoea.
- Jinsi kelele za dunia zinavyoweza kuathiri uwezo wa kusikia sauti ya Mungu.
- Hatari ya kuishi maisha ya kidini bila msimamo wa maisha ya kiroho
- Umuhimu wa kuishi kwa imani hai inayozalisha matendo ya haki
- Njia za kukuza imani yako kwa kusikia na kulitii Neno la Mungu kila siku
Lengo la Kitabu: Nini kilinisukuma kuandika kitabu hiki. Malengo makuu ya kuandika kitabu hiki ni:
- Kumsaidia msomaji kutambua na kushinda ushawishi wa dunia hii.
- Kuamsha tena kiu ya kusikia sauti ya Mungu bila kuvurugwa.
- Kukuza uhusiano wa kibinafsi na Mungu kwa njia ya imani.
- Kuweka msingi wa kiroho thabiti unaostahimili misukosuko ya maisha.
Ikiwa unataka Kukuza imani yako na kuibakiza salama ingawa dunia ina changamoto nyingi, basi kitabu hiki kitakufaa sana na kitakuwa msaada kwako.
Recommended for you

Safari ya Imani
TZS 4,000