Machungu ya Usaliti
HEARTBREAK 💔💔Sehemu ya 01
Ilikuwa ni mchana nikijiandaa kwenda discussion kwa sababu wiki ijayo nilikua na mitihani ya kumaliza chuo mtoto nimependeza ukiangalia na shepu ninalo , kabla sijaenda discussion kaka alinipa flash niipitishe saluni kwake,nikaichukua na kuondoka zangu.
Saluni hapakuwa mbali na nyumbani,nilifika saluni na kumkuta kinyozi nilimkabidhi na kuanza kupiga hatua aliniita mbona umsalimii rafiki yangu.
Ndipo nikamuona kijana amekaa anabani CD ya muvi mwanzo sikumuona kutokana na haraka zangu sababu kinyozi alichukua flash nje ya saluni.
Nilimsalimia kwa kupunga mkono “habari ”alitabasamu 😊 kisha akaitikia “salama” nami nikaondoka zangu.
Nilifika discussion nilikuta wenzangu ndio wameanza niliungana nao paka sa 12 kasorobo ndipo nilipoanza safari ya kurudi nyumbani.
Nafika maeneo ya saluni kinyozi aliinita “nancy,njoo ”nami bila maringo nilianza kupiga hatua kumwelekea, kisha tukaanza kupiga stori za hapa na pale kwa sababu alikuwa mchangamfu sana.
“Aroni naomba nikimaliza mitihani yangu niwe nakuletea kashata unaniuzia”aroni alikubali bila shida, mara akaja yule kaka aliekuwa akibani CD ya muvi Aroni akamuuliza “vipi Idriss”hapo ndipo nikalifahamu jina lake, Idriss alijibu kuna mteja anataka huduma ya kunyolewa.
Mungu alijaria nikafanya mitihani nikamaliza nikaanza kupika kashata na kupeleka saluni kwani kulikuwa na watoto wengi walikuwa wanapenda kukaa pale nami ndiyo nikajionea fursa ata ya kupata mia mia .
Basi siku zikaenda nikaanza kuzoeana taratibu na Idriss sababu ya kupeleka kashata pale kila siku.
Kama unavyojua wanaume walivyo alianza kuonyesha ishara za kunitaka ♥️♥️, moyoni nilijisemea siwezi kua na muislamu ata siku moja nataka mkristo mwenzangu .
Hatimaye alinifungukia kuwa ananipenda
Others Also Bought