Sio Sababu ya Kuvunja
Downloadable file
How to buy
Sio Sababu ya Kuvunja ni kitabu kinacho husu Sheria,Jamii na Maisha.
Kutojua sheria sio sababu ya kuvunja sheria. Hii ni kanuni muhimu katika mfumo wa sheria, ambapo mtu hawezi kuvunja sheria kisha akajitetea kuwa hakufahamu kuwa kitendo alichokifanya ni kinyume na sheria.
Mzee Majanida, akiwa miongoni mwa wazee wa chama cha siasa katika mji wa Kilongelea, anapanga mipango yeye pamoja na wazee wenzake kuhakikisha Mheshimiwa Kipaumbele anapata nafasi ya kuliongoza jimbo la Kilongelea kwa mara nyingine. Mipango ya wazee wa chama hiki ilipelekea uvunjifu wa haki na sheria katika uchaguzi wa wabunge katika nchi ile. Vilevile, ilipelekea vifo vya watu wasio na hatia katika mji ule.