Tambua majira na nyakati ili ufanikiwe
Katika safari ya maisha, kila mtu anakutana na nyakati tofauti za kupanda na kushuka, furaha na huzuni, kupokea na kusubiri. Hata hivyo, changamoto kubwa ambayo wengi wanakutana nayo ni kujua namna ya kutambua majira wanayopitia, na pia namna ya kujipanga kulingana na yale ambayo Mungu amepanga kwa wakati huo. Kitabu hiki, Tambua Majira na Nyakati ili Ufanikiwe, kimeandikwa kwa kusudi kuu la kumsaidia msomaji kugundua hekima ya Mungu kuhusu nyakati, na namna ya kuishi kwa ufanisi ndani ya kila majira.
Biblia inatufundisha wazi kuwa maisha yetu yamepangwa kwa majira tofauti. Kama inavyojulikana katika Mhubiri 3:1, “Kwa kila jambo kuna majira yake, Na wakati kwa kila kusudi chini ya mbingu.” Maandiko haya kutoka kitabu cha Mhubiri yanatufundisha kwamba hakuna jambo au tukio linalotokea kwa bahati mbaya. Kila jambo lina muda wake maalumu. Lakini swali ni: Je, tunalitambua hilo? Tunajua lini ni wakati wa kupanda, na lini ni wakati wa kuvuna? Lini ni wakati wa kusubiri, na lini wa kutenda?
Mafanikio halisi ya maisha haya yanategemea zaidi uwezo wa mtu kutambua kile Mungu anachofanya katika majira mbalimbali, na kujiweka sawasawa na hilo. Kupitia kitabu hiki, utajifunza jinsi ya kutambua nyakati za Mungu katika maisha yako,
Ni matumaini yangu kuwa kitabu hiki kitakuwa msaada mkubwa kwako, kukufungua macho ya kiroho, na kukuongoza katika njia ya mafanikio katika maisha yako. Mungu anataka usimame imara kila wakati, ukijua linapokuja giza au nuru, mvua au kiangazi, ukame au utele na kuishi kwa hekima inayotoka juu.
Karibu tujifunze pamoja.
Recommended for you



