Skip to main content
DL Bookstore
  • Home
  • Get books
  • Author services
  • Courses
  • Blog
  • Support

Tabia 5 zinazoleta mafanikio kwa muandishi

February 17, 2021 at 6:51 pm,


Kila muandishi wa vitabu hutaka kufanikiwa lakini mafanikio huchagizwa na tabia anazokuwa nazo muandishi mwenyewe. Kuna tabia tano ambazo muandishi akiwa nazo basi mafanikio huja yenyewe.


1. Andika kila siku. Kuandika kila siku si jambo dogo na pengine wajiuliza, β€œhili linawezekanaje?”. Lakini unaweza kutenga dakika 5 mpaka 10 kila siku ukaandika, hata kama ni kitu kidogo kiandike. Unaweza kuwa na dakika hizo asubuhi, usiku au mchana wakati. Misuli yako kama muandishi hupashwa kila siku unapoandika.

2. Soma kadri unavyoweza. Huwa wanasema muandishi mzuri ni msomaji mzuri. Soma vitabu vya waandishi mbalimbali, hata vile ambavyo sivyo vya aina unayooandika wewe. Unapofanya hivyo unapata ladha mbalimbali za waandishi wengine na itakufanya kuwa bora zaidi

3. Jiwekee malengo yaliyo wazi. Utapimaje mafanikio yako kama huwezi malengo? Weka malengo yaliyo wazi, yanayopimika.Unaweza kutimiza malengo unayojua, na ambayo unaweza kujikumbusha.

Soma pia: Ufanye Nini Uzinduzi Wa Kitabu Chako Unapofeli?

4. Penda kutumia teknolojia. Muandishi lazimia ujenge tabia ya kwenda na teknolojia. Si muda wote utatumia Microsoft Word kuandika, nenda playstore au appstore na weka evernote. Huwezi kutembela na kalenda kila mahali ili kujikumbusha malengo yako, jizoeze kutumia google kalenda. Zipo teknolojia nyingi mno, jizoeze kuzitumia.

5. Maliza kila unachoanza. Uwe na tabia ya kumalizia vitabu unavyoandika. Najua ni ngumu hii, lakini inawezekana. Kumbuka nguvu uliyoweka ulipoanza kuandika, ukiishia njiani umepoteza muda na nguvu yote uliyoweka. 

Tembelea HAPA kusoma kozi za uandishi wa vitabu bila gharama yoyote



Recent Posts

  • Umechoka na Minyama Uzembe? Suluhisho la Kupungua Uzito Limepatikana!
    17 Apr, 2025
  • Vitabu Bora vya Pasaka vya Kukuimarisha Kiroho – Vinapatikana Sasa DL Bookstore
    11 Apr, 2025
  • 4 Benefits of Selling Your Book Through DL Bookstore
    20 Mar, 2025
  • Download Entrepreneurship Books (PDF) in Swahili
    10 Feb, 2025
  • Download Nine (9) Must-Read Books for Girls and Women πŸ“šβœ¨
    4 Feb, 2025
  • A Tanzanian Platform for Selling Books Online
    4 Feb, 2025
  • Jinsi ya Kuandika Caption Inayochochea Mauzo ya Kitabu Chako
    23 Nov, 2024

selling_book-1.png

Enroll in 100% free courses

100% free courses on writing, publishing, and marketing of books. Time to dive in!

Start learning β†’

Cart

Cart is empty.

  • Home
  • Get books
  • About us
  • Author services
  • Blog
  • Support
  • Client portal
DL Bookstore Β© 2025. All rights reserved.