Kusudi la maisha yako
Upekee wa kila mwanadamu aliyekwisha kuishi hapa duniani, anayeishi sasa na atakayeishi baada ya sasa umethibitishwa kisayansi kwa kutumia alama za vidole.
Kila mtu ana alama za vidole za kipekee ambazo hazifanani na za mtu mwingine. Hata mapacha wa kufanana wanatofautiana katika alama za vidole.
Yawezekana ulizaliwa pasipo matarajio ya wazazi wako, na matarajio ya ulimwengu wote. Lakini haukuumbwa bila kusudi la pekee na Mungu. Uliumbwa uzae, uongezeke, utiishe, utawale na umiliki kwa namna iliyo ya kipekee. Uliumbwa kutimiza kusudi la kipekee kabisa, la Mungu.
Kwenye kitabu hiki, utafundishwa kwa Neno la Mungu, sababu ya wewe kuwa hapa duniani. Utajifunza kwamba, hakuna mtu aliyekuja hapa duniani kusindikiza wengine, au kusaidia wengine. Maana Mungu alipokuumba mtu kwa namna ya pekee, hakuwa anabahatisha.
Safari nami kwenye safari hii ya kujifunza, “Kusudi la Maisha Yako”
Recommended for you


