Mjue Yesu
Kumjua Yesu Kristo ni kwa muhimu kwa ajili ya kukujenga wewe mwana wa Mungu katika kuwa na mahusiano naye ya karibu zaidi.
Kuna tofauti kati ya kujua, kufahamu na kuelewa. Pia, kumjua Yesu si kujua habari za Yesu, si kufahamu historia ya Yesu, si kuelewa kwa akili maandiko kwenye Biblia yanayomwongelea Yesu.
Kumjua Yesu ni kuungana naye binafsi. Kumpokea Yesu binafsi ndani ya moyo wako. Kupokea nuru ya Yesu na makusudi ya kuja kwake hapa duniani.
Macho ya moyo wako yatiwe nuru, upate kufahamu tumaini la mwito wa Yesu, na utajiri wa utukufu wake aliowarithisha watakatifu, na uweza wake uliozidi sana kuwaelekea wanaomwani, uweza huo umo ndani ya wanaomwamini, ni uweza uliomfufua Yesu toka kwa wafu (Waefeso 1:17-20).
Mungu wa utukufu akupe roho ya hekima na ya ufunuo katika kumjua yeye. Usiishie tu kufahamu habari za Yesu kupitia watu, bali yeye mwenyewe akupe kububujika tokea ndani mwako.
Yesu Kristo ni fumbo. Ili kumjua Yesu Kristo ni lazima yeye mwenyewe akufumbulie fumbo hilo.
Kutokana na ukweli kwamba watu wengi hawamfahamu Yesu Kristo, tena hata miongoni mwa wale wanaomwamini; hata kupelekea kubabaika pale wanapokutana na changamoto za maisha yao ya kila siku nimeona vyema kuandika habari za Yesu Kristo kama vile Neno la Mungu linavyotuelekeza.
Kutomfahamu Yesu si tatizo la watu wa siku za sasa tu. Ni tatizo ambalo lilikuwepo tokea siku nyingi, hata wakati Yesu mwenyewe alipokuwapo hapa duniani.
Recommended for you

