Mwamini Mungu
Pasipo imani, haiwezekani kumpendeza Mungu, lakini imani hiyo ni lazima iwe na msingi thabiti kabisa kwenye ukweli unaopatikana katika NENO la Mungu. Imani isiyo tokana na msingi wa NENO la Mungu husababisha madhara makubwa sana kwa waamini na jamii inayowazunguka.
Undani wa msingi wa imani kwa Mungu ni kuamini kwamba “yeye (Mungu) yuko”. Tafsiri nyingine imeonyesha neno hili kuwa na maana kwamba “yeye ndiye” kama vile alivyojitambulisha alipokutana na Musa.
Mungu alimwambia Musa, “Ukawaambie NDIMI (maana yake yuko), amenituma kwenu”. Mungu alijitambulisha kama “Ndimi niliyeko”. Hivyo, kila anayemwamini Mungu ni lazima aweke mhimili wa imani yake kwenye uelewa kwamba Mungu “Ndiye aliyeko”.
“Ndimi niliyeko” ni utambulisho wa kwanza kabla ya “ndimi ninayefanya mambo kadhaa” na “ndimi ninayemiliki vitu kadhaa”. “Ndimi niliyeko” habadiliki kutokana na mambo yanayobadilika kama mazingira ya duniani. “Ndimi niliyeko” yuko hivyo hivyo na hatobadilika.
Usomapo kitabu hiki ni vizuri kabisa ukaoanisha yale utakayoyasoma na NENO linalopatika kwenye Biblia yako, na ukamshirikisha Roho Mtakatifu akupe ushuhuda juu katika yale yaliyoandikwa humu.
Recommended for you

