Sauti ya Imani
2 Timotheo 4:3-4 “Maana utakuja wakati watakapoyakataa mafundisho yenye uzima, ila kwa kuzifuata nia zao wenyewe watajipatia waalimu makundi makundi, kwa kuwa wana masikio ya utafiti, nao watajiepusha wasisikie yaliyo kweli, na kuzigeukia hadithi za uongo” (KJV)
2 Timotheo 4:3-4 “Maana wakati utakuja watakapokataa kuyakubali mafundisho yenye uzima. Badala yake, ili kutimiza tamaa zao wenyewe, watajikusanyia idadi kubwa ya walimu wapate kuwaambia yale ambayo masikio yao yanayowasha yanatamani kusikia. Watakataa kusikiliza kweli na kuzigeukia hadithi za uongo.” (NIV)
Kile kizazi ambacho mtume Paulo alikisema, sasa kimeshawadia, ndio hiki tulichonacho sasa. Kizazi ambacho hakitaki kabisa kusikia mafundisho ambayo yana uzima ndani yake bali wanachagua kusikia mafundisho wanayoyataka wao ambayo hayana uzima bali yanawaburudisha tu.
Kutokana na kuwa na sauti nyingi za kigeni katika nyakati hizi za mwisho imewafanya wakristo wengi kupoteza imani zao za kweli kwa kuzitoa kwa Mungu wao anayeweza kuwaokoa na
kuzipeleka kwa vitu visivyoweza kuokoa.
Kwa kuwa chanzo cha Imani ni Neno la Mungu, kuna watu wengi wamejiingiza kufundisha neno kwa jina la wahubiri lakini hawahubiri neno la Kristo bali mambo ya kuhamasisha tu watu kujipambania maisha yao, na hivyo imepelekea wakristo wengi kuzigeukia sauti hizo ambazo zimeua kabisa imani hiyo.
Na hata wale wanaosikia neno la kweli bado wanashindwa kuamini na hata wale wanaoamini nao wanashindwa kufanya matendo ya imani na hivyo wengi kushindwa kuyaona matokeo ya imani yao.
Kitabu hiki ni kwa ajili ya kuhuisha shauku iliyopotea ya kusikia Neno la Mungu lenye uzima na kuzaa tena imani ndani yako.
Others Also Bought