Kuenenda Kwa Kuukomboa Wakati
Matumizi sahihi ya wakati (muda) ni changamoto kwa watu wa rika zote. Hivyo imepelekea kutokea kwa matokeo yasiyotarajiwa katika nyanja mbalimbali za maisha.
Kitabu hiki kimekusudiwa kwa watu wa rika zote na jinsi zote, pia kitabu hiki kimekusudia kuleta utatuzi katika matumizi sahihi ya muda ili kufikia hatima nzuri ya kiroho na kimwili, pia kinaelezea mapenzi ya Mungu kuhusu muda, na zaidi kinatusaidia kuzipata Siri zilizojificha katika kuukomboa wakati.
Matumizi sahihi ya muda ni moja ya vigezo ambavyo Mungu ameviweka ili mwanadamu aweze kufikia mafanikio yake kiroho, kimwili, kiakili na kiafya pia. Kupitia kitabu hiki utapata kujifunza kufanya kila jambo kwa wakati wake kwa kuzingatia mpango wa Mungu katika Muda, utapata pia kuelewa sababu za kutumia muda ipasavyo, faida ambazo mtu atazipata kwa kufika eneo husika kwa wakati pamoja na hasara za kutofika katika eneo kwa wakati.
Utapata kujifunza siri zilizojificha za namna ya kuukomboa wakati n nini ufanye ili ufike kwenye eneo unalohitajika kwa wakati unaofaa. Kupitia kitabu hiki utaweza kubadilisha mtazamo wako kuhusu kuukomboa wakati, kwa kutazamia mabadiliko chanya hata kuweza kuifikia hatima yako. Jipatie nakala yako sasa.
Others Also Bought