Skip to main content
DL Bookstore
  • Home
  • Get books
  • Author services
  • Courses
  • Blog
  • Support
  • All books
  • Offers
  • Swahili books
    • Dini
    • Fasihi
    • Maendeleo binafsi
    • Malezi
    • Ndoa na mahusiano
    • Uchumi na biashara
    • Uongozi na usimamizi
    • Vitabu vya kiada
  • English books
    • Business and finance
    • Literature
    • Parenting and relationships
    • Personal development
    • Religion and spirituality
    • Textbooks
  • Children's books
  • Online courses
  • Free books
  • Get books
  • Swahili books
  • Dini
  • Zijue nyakati na majira katika mpango wa Mungu

Zijue nyakati na majira katika mpango wa Mungu

TZS 7,000

Hardcopy Softcopy
Add to cart  

Kila zama na watu wake, kila nyakati na matendo yake, naam kila matendo ni matokeo ya mapokeo ya mafunzo na hekima walizonazo watu wa zama husika. Kama ningeliweza, ningelipaza sauti yangu isikike na watu wote waweze kusoma kitabu hiki. Kitabu hiki, “Zijue nyakati na Majira katika mpango wa Mungu”, kimenifanya nizidi kumshukuru Mungu kwa Baraka na Neema ya kutupa Mtumshi wake, Eng. Bujo Mwakapalila (Mwandishi) ambaye amekuwa mstari wa mbele katika kuilisha jamii Neno la Mungu na kuwapa watu kiu ya kutaka kula Mkate wa uzima.

Kitabu hiki kina sura Ishirini na mbili (22) ambazo zinatoa mafafanuzi kuanzia ‘Nyakati za wamataifa’ (Sura ya kwanza) hadi kufikia ‘Mambo mapya ya milele’ (Sura ya Ishirini na mbili). Katika sura hizi zote, mwandishi ametumia marejeo ya Biblia kama rejea yake kuu ya kihistoria na jumbe zote za kuelimisha. Mwandishi amefanya nukuu mbalimbali kutoka kwenye maandiko ya Biblia ili kukuwezesha kuelewa zaidi misingi ya elimu utakayoipata ndani ya kitabu hiki, na zaidi sana, kitabu hiki kimetumia zaidi lugha/Kiswahili cha ki-Biblia ili kuzidi kuzielekeza fikra zako kupata mafafanuzi ya kina.

Kitabu hiki kitafanyika kuwa nguzo, msaada na jibu la baadhi ya maswali yako ambayo umekuwa ukijiuliza kwa muda mrefu. Ni matumaini yangu kuwa kitakufunza na kitakupa wasaa wa kufanya tathmini ya kina ya maisha yako kama moja ya wanafunzi wa Neno la Mungu. Uwapo na maswali, mrejesho ama mawazo ya aina yoyote, nakushauri usiache kuwasiliana na Mwandishi kupata maelezo ya kina.

Kitabu hiki chafaa kwa watu wote wanaoishi sasa na watakaokuwapo katika
nyakati zijazo.


Recommended for you

Ushindi katika hali ngumu
Ushindi katika hali ngumu
TZS 7,000 TZS 6,500
View options
HILI NI NENO LA KUFAA KWAKO - Siku 21 za kukua, kujijenga na kujiimarisha kiroho
HILI NI NENO LA KUFAA KWAKO - Siku 21 za kukua, kujijenga na kujiimarisha kiroho
TZS 9,999 TZS 7,500
View options
Utimilifu wa majuma 70 ya unabii wa kitabu cha Danieli na unabii wa siku za mwisho
Utimilifu wa majuma 70 ya unabii wa kitabu cha Danieli na unabii wa siku za mwisho
TZS 7,000
View options
Agano Lililo Bora
Agano Lililo Bora
TZS 9,999 TZS 6,999
View options

Cart

Cart is empty.

  • Home
  • Get books
  • About us
  • Author services
  • Blog
  • Support
  • Client portal
DL Bookstore © 2025. All rights reserved.