Usijidharau Ulizaliwa na Unaishi kwa Kusudi Maalumu
Kitabu hiki chenye kichwa “USIJIDHARAU, ULIUMBWA NA UNAISHI KWA KUSUDI MAALUMU” ni zawadi ya kipekee sana na yamkini katika vitabu kadhaa ulivyowahi kuvisoma hiki ni cha tofauti sana kwani kimebeba ujumbe wa thamani sana kwako.
Ndani ya kitabu hiki utajifunza mambo mengi sana. Ikiwemo maana ya kusudi, ishara za mtu asiyejua kusudi lake, uhusiano kati ya kutolijua kusudi na Kujidharau, dhana kuu kuhusu kusudi na Kujidharau.
Pia utajifunza thamani ya uhai ulionao, namna ya kutambua kusudi, mchakato wa kutumikia kusudi, gharama za kutumikia kusudi, hasara za kutoliishi kusudi, faida na ushindi unaopatikana kwa kuliishi kusudi kwa uaminifu na ukamilifu.
Nikualike katika safari ya kujitambua ili ung'are kwani lengo la wewe kuwa hai ni ili ung'are na kudhihirisha utukufu wa Mungu nje ya hapo ni kuamua kufubaa na maisha yatakupa kila sababu ya kuanza kujidharau, kujikatia tamaa na hata kutokuona thamani ya uhai wako.
Kulingana na hali ya sasa ya dunia, watu wengi wamekata tamaa, hawaoni thamani ya uhai wao, matukio ya watu kujiua yanazidi kuongezeka na wengine kujiona hawafai na kujidharau.
Karibu sana tushirikiane haya maarifa ya thamani mno uweze kutambua kusudi la Kuumbwa, kuzaliwa na kuishi na uachane na maisha ya kujidharau, kujikatia tamaa na kujiona haufai.
USIJIDHARAU, UHAI WAKO NI WA THAMANI MNO.
Recommended for you



