Skip to main content
DL Bookstore
  • Home
  • Books
  • Publish
  • Sell
  • Courses
  • Blog
  • Support

Makosa 4 Wanayofanya Waandishi Wanapotangaza Vitabu Vyao

November 16, 2020 at 2:31 pm,


Kwa waandishi wengi, kuuza vitabu ni kazi ngumu kuliko kuandika. Kujifunza kutangaza na kuuza kitabu ndiyo msingi wa mafanikio kwa muandishi yeyote yule. Tumekuandikia makosa 4 ambayo waandishi wengi wanafanya wanapotangaza  vitabu vyao na wanajikuta mauzo yao ya vitabu yapo chini.


1. Kutangaza kitabu chako kwa kila mtu. 

Lazima ujue kitabu chako ni mahsusi kwa kundi lipi la wasomaji ili juhudi zako za kutangaza iweze kuzaa matunda.

Tunapowauliza waandishi, umeandika kitabu chako kwa kundi lipi la wasomaji?, wengi hujibu “nimewalenga vijana zaidi” lakini kwa bahati mbaya jibu kama hili linaonyesha udhaifu katika namna mbili; mosi, si kila kijana atasoma kitabu chako, hivyo unakuwa na mategemeo yasiyo halisi, pili, utapoteza muda na fedha yako kutangaza kitabu chako kwa kundi la watu wasio sahihi wasioweza kununua.

Kutangaza kitabu ni kuwaambia kundi la wasomaji wako uliowalenga kusoma kitabu chako. Fikiria mapema kuhusu wasomaji uliowalenga kusoma kitabu chako hata kabla ya kumaliza kuandika kitabu

2. Huna orodha ya baruapepe za wasomaji wako. 

Kutangaza kitabu chako kwa kuwatumia baruapepe wasomaji wako ni njia isiyo na gharama na huleta matokeo chanya. Tunashangazwa mno na waandishi wengi ambao bado hawana orodha ya baruapepe ya wasomaji wao.

Kama huna orodha hii, mahali pa kuanzia ni kuwa na blogi yako kama muandishi ambayo itakusaidia kukusanya baruapepe za wasomaji, kisha fungua akaunti ya mailer au mailchip kutuma jumbe zako kwa wasomaji.

Get a Free PDF

Enter your email to get a free PDF "Hatua 6 rahisi za kuandika kitabu"

Thank you!

Go to your email inbox to download your free PDF

.

3. Unajitengenezea jalada la kitabu mwenyewe. 

Wasomaji hawanunui vitabu ambavyo jalada lake halivutii na linaonekana ni kama mtu alikuwa akijifunza au akijaribu. DL Bookstore tumewasaidia waandishi wengi kupata jalada la kitabu lenye muonekano bora na linaloongeza mauzo ya kitabu chako. Wasiliana nasi tukusaide na wewe

Pia unaweza kusoma: Maswali 5 ya kujiuliza kama jalada la kitabu linafaa

4. Unaona huwezi kutoa kitabu chako BURE au kutoa ofa ya punguzo la bei. 

Baada ya miezi mitatu, kuwa na siku 5 za kuuza kitabu chako kwa punguzo au wape wasomaji wako bure. Angalizo hapa; ni wasomaji walio kwenye orodha yako ya baruapepe tu!.

Kutoa ofa kwa wasomaji wako huongeza idadi ya wasomaji wapya watakaojua kazi zako na wataweza kununua vitabu vingine ulivyoandika. Ofa ni sehemu ya kuwa karibu zaidi na wasomaji wako na watajua kuwa unawajali. 


 Nunua kitabu cha kusoma mwezi huu  Huduma zetu kwa waandishi 




Recent Posts

  • Mapitio ya Kitabu: Mimi Ashraf — Riwaya Inayokupeleka Ndani ya Nafsi ya Mwanadamu
    3 Jun, 2026
  • Vitabu 6 Bora vya Uwekezaji na Uhuru wa Kifedha kwa Kiswahili
    20 May, 2026
  • Vitabu Bora vya Biashara Kwa Kiswahili PDF
    18 May, 2026
  • Nukuu 24 Bora kutoka kitabu cha Hisa, Hatifungani, Vipande
    8 Apr, 2026
  • Book review: Hisa, Hatifungani, Vipande - Uwekezaji kwa Ukuaji wa Mtaji na Kipato Endelevu
    6 Apr, 2026
  • Siku ya Wanawake: Sherehekea Siku Yako na Maarifa
    7 Mar, 2026
  • Unahitaji nini ili uuza kitabu chako dlbookstore.com
    2 Mar, 2026

Categories

  • Book Recommendations
  • Book Reviews
  • Help & Support
  • Offers and discounts
  • Reading Habits & Tips
  • Writing, Publishing & Author Support

Start selling your book or course on our website — reach more readers

You will enjoy high book visibility, get paid on time and receive a monthly sales report straight to your inbox.

Start selling →

Cart

Cart is empty.

  • Home
  • Books
  • Return policy
  • About us
  • Publish
  • Sell
  • Blog
  • Support
DL Bookstore © 2026. All rights reserved | Made with ❤️ in Tanzania.