JINSI YA KUANDIKA ‘KUHUSU KITABU’ INAYONASA WASOMAJI WASOME KITABU CHAKO

Kama msomaji wa vitabu, ni jambo gani la kwanza huwa unaangalia kwenye kitabu baada ya kuona jalada la kitabu? Iwe upo kwenye duka la vitabu au unanunua kitabu mtandaoni, utaangalia kuhusu kitabu – maelezo yanayohusu kitabu. Kama muandishi wa kitabu ni lazima ujue kuandika kuhusu kitabu ambayo itamnasa msomaji asome kitabu chako. Kama ulikuwa hujui, hakuna kitu kinachouza kitabu chako kama kuhusu kitabu iliyoandikwa vizuri.
Maelezo ya kuhusu kitabu siyo ufupisho wa nusu kurasa wa kitabu chako, la! Ni tangazo lako la kumfanya msomaji anunue kitabu. Kwahiyo inabidi ufikirie kuanzia sasa kuhusu kitabu kama nyenzo ya wewe kuuza kitabu. Kuna mambo 4 ya kuzingatia unapoandika kuhusu kitabu;
1. Iwe fupi.
Wastani wa maneno unaofaa unapoandika
kuhusu kitabu ni maneno 150 mpaka 250 tu, na kwa nadra sana, yakizidi, basi
yawe maneno 300. Usiwachoshe wasomaji kusoma maelezo marefu yasiyoongeza kitu.
2. Andika katika nafsi ya tatu.
Hata kama kitabu
chako umeandika katika nafsi ya kwanza, unapoandika kitabu tumia nafsi ya tatu.
Mfano, “alikimbia sana lakini mbio zake hazikufua dafu, lile joka kubwa jeusi
lilimfikia na…”
3. Iwe chambo.
Weka ujuzi wako, sentensi ya kwanza
tu imnase msomaji. Usiweke blah blah zisizo na maana kwani msomaji hatanaswa
kusoma zaidi na kisha kununua kitabu chako. Kuhusu kitabu ni tangazo!
4. Usitumie maneno magumu.
Unapoandika kuhusu
kitabu, tumia maneno marahisi, yenye maana ya moja kwa moja na siyo kumfanya
msomaji awe kama anazunguka mbuyu kutafuta maana ya maneno. Lengo ni kuuza
kitabu siyo kuonyesha ujuzi wa maneno.
NUNUA WEKA ODA