Skip to main content
DL Bookstore
  • Home
  • Books
  • Publish
  • Sell
  • Courses
  • Blog
  • Support
  • Sign in

Recent Posts

  • MFAHAMU MWANDISHI: DAUDI LUBELEJE - Mwandishi nyuma ya vitabu 14
    5 Sep, 2026
  • Vitabu 25+ vya Biashara, Fedha na Uchumi
    27 Aug, 2026
  • Book review: Amazing Animal Coloring Book for Kids
    11 Jul, 2026
  • Mapitio ya kitabu: Utambulisho Wako Katika Kristo
    21 Jun, 2026
  • Mapitio ya Riwaya: Mimi Ashraf
    3 Jun, 2026
  • Vitabu 6 Bora vya Uwekezaji na Uhuru wa Kifedha kwa Kiswahili
    20 May, 2026
  • Vitabu Bora vya Biashara Kwa Kiswahili PDF
    18 May, 2026

Categories

  • Book Recommendations
  • Book Reviews
  • Help & Support
  • Offers and discounts
  • Reading Habits & Tips
  • Writing, Publishing & Author Support
  • Author Spotlight

Start selling your book or course on our website — reach more readers

You will enjoy high book visibility, get paid on time and receive a monthly sales report straight to your inbox.

Start selling →

MFAHAMU MWANDISHI: DAUDI LUBELEJE - Mwandishi nyuma ya vitabu 14

September 5, 2026 at 9:19 pm,

MFAHAMU MWANDISHI: DAUDI LUBELEJE - Mwandishi nyuma ya vitabu 14

Unaweza kuandika vitabu 14 kwa sababu tu unapenda kuandika? Kwa Daudi Lubeleje, jibu ni ndiyo.

Daudi alianza safari yake ya uandishi wa vitabu mwaka 2016, na kitabu chake cha kwanza kilikuwa Mambo 7 Usiyoyajua Kuhusu Dhambi. Tangu wakati huo, ameendelea kuandika vitabu mbalimbali vinavyogusa imani, maendeleo binafsi, uandishi, biashara na uwekezaji.

Kitabu chake cha hivi karibuni ni Hisa, Hatifungani,Vipande: Uwekezaji kwa Ukuaji wa Mtaji na Kipato Endelevu, kinachozungumzia uwekezaji na namna ya kujenga mtaji na kipato endelevu.

Vitabu alivyoandika

  1. Mambo 7 Usiyoyajua Kuhusu Dhambi
  2. Mduara wa Dhambi
  3. Chochea Kipaji Chako
  4. Mambo Muhimu kwa Mwalimu wa Biblia Unapoandaa Somo
  5. Ushindi katika Hali Ngumu
  6. Sadaka ya Fungu la Kumi ni Nini?
  7. Uandishi wa Kitabu Kinachouzika
  8. Tumia Fursa Tengeneza Biashara
  9. Kutoka Kuandika Mpaka Kuuza Kitabu
  10. Naandikaje Kitabu?
  11. HILI NI NENO LA KUFAA KWAKO – Siku 21 za Kukua, Kujijengana Kujiimarisha Kiroho
  12. Mbinu Rahisi za Kuandika Kitabu
  13. Utumishi Unaotimiza Mapenzi ya Mungu
  14. Hisa, Hatifungani, Vipande: Uwekezaji kwa Ukuaji wa Mtajina Kipato Endelevu

Lakini siri ya Daudi kuandika vitabu vingi si kwamba ana mbinu fulani ya kichawi. Anapenda kuandika.

Anapokaa kuandika, anaweza kutumia masaa mengi bila hata kutambua muda umepita. Kwake, kuandika si jambo analolazimisha kufanya; ni kitu anachofurahia.

Mbali na uandishi wa vitabu, Daudi ni mwanzilishi wa DaudiPages Academy, inayowasaidia watu kujifunza mambo mbalimbali kuhusu uandishi wa vitabu—kuanzia kupata na kuendeleza wazo, kuandika kitabu, hadi kukitoa na kukiuza. Pia hutoa kozi mbalimbali za uandishi pamoja na one-to-one mentorship kwa waandishi.

Na anapokuwa si kwenye uandishi? Anapenda kusoma vitabu vya waandishi wengine na kupiga gitaa.

Huyo ndiye Daudi Lubeleje—mwandishi, mwalimu wa waandishi, msomaji wa vitabu na mtu anayefurahia sana mchakato wa kuandika.

Ungependa kusoma vitabu vyake?

DL Bookstore inakualika kuvipata vitabu vya Daudi Lubeleje.

Kama ungependa kusoma zaidi ya kimoja, chagua vitabu unavyotaka kwenye bundle yako na tutakupatia punguzo kubwa la bei. Tuandikie kwenye comment au bofya hapa kuwasiliana nasi

Je, umewahi kusoma kitabu cha Daudi Lubeleje? Ni kipi?



Cart

Cart is empty.

  • Home
  • Books
  • About us
  • Publish
  • Sell
  • Blog
  • Support
  • Sign in
DL Bookstore © 2026. All rights reserved | Made with ❤️ in Tanzania.